0
Rais mpya wa Gambia Adama Barrow, amewasili nchini humo kuchukua hatamu za uongozi, kufuatia kuondoka madarakani kwa rais wa mda mrefu Yahya Jammeh
Barrow aliapishwa wiki iliyopita nchini Senegal wakati viongozi wa kieneo walipokuwa wakimshawishi Jammeh kuondoka madarakani.
Maelfu ya watu walifurika katika barabara za mji mkuu wa Gambia Banjul kumlaki rais huyo mpya.
Wanadiplomasia walimtaka Barrow arudi mara moja nyumbani kuepuka pengo la uongozi.
Taarifa zinasema Barrow atakaa katika makaazi yake wakati ukaguzi ukifanywa katika ikulu kutambua hatari yoyote kufuatia kuondoka kwa Yahya Jammeh kwenda uhamishoni Guinea ya Ikweta.
Maelfu kadhaa ya wanajeshi wa mataifa ya Afrika magharibi wanasalia Gambia wakati kukiwa na taarifa kuwa wafuasi waovu wa Jammeh wamo miongoni mwa vikosi vya usalama nchini.

Post a Comment

 
Top