0


     PHONE NO:+255624031936 or+255768550136                                                                                 TOVUTI:www.sitenewztanzania,blogspot.com                                                                              
                                                                                         Na mwandishi wetu magdalena marko


                                                    mchungwa na maua yake
Mpenzi msomaji wa makala ya AFYA YA JAMII natumai U-mzima wa afya njema na unaendelea vizuri na majukumu yako ya kla siku nakusihi ambatana nami katika safu hii ili kujua mambo kadha wa kadha kuhusu matunda ambapo kwa siku ya leo tutaangalia tunda aina ya chungwa pamoja na faida zake.
 Chungwa ni tunda linalostawi ulimwenguni kote , lakini haswa tunda hili lilianza kusini mwa bara la Asia, huku likilimwa sana huko nchini China.
Kumbuka kuwa hata chungwa moja tu ukila lina kidhi yale mahitaji muhimu ya mwili ya kila siku (daily requirement), iwe chungwa lenyewe au juisi yake halisi
Inasadikika kuwa Chungwa lina kiwango cha juu cha vitamin C, huku nyama /ngozi nyeupe iliyozunguka kati ya ngozi ya nje na tunda lililomenywa ni chanzo kizuri cha madini ya ‘calcium.’
Endapo unasumbuliwa na magonjwa magonjwa mbalimbali pamoja na mafua waweza kuongeza maji ya moto katika juisi ya chungwa kisha kuyanywa.
 Majani ya mchungwa yakipondwa na kisha kuchanganywa na maji ya moto pamoja na asali kidogo, kwa ujumla mchanganyiko huo hutumika kama dawa ya kikohozi. 
Kama  maua makavu ya mchungwa yakisagwa nakuchanganywa katika maji ya moto ni dawa ya shinikizo la mishipa ya fahamu. 
Huku maganda yake yakisuguliwa usoni huwa ni dawa ya chunusi. Pamoja na hayo, kwa ujumla juisi ya machungwa husaidia ugonjwa wa pumu, matatizo ya kifua, kusafisha damu, kupooza, kuungua, matatizo ya meno pamoja na beriberi.
Virutubisho vya Magnesi (Magnesium) na ‘hesperidin’ vilivyomo kwenye chungwa, husaidia kuondoa tatizo la shinikizo la damu la juu (high blood pressure), hivyo machungwa ni mazuri kwa wagonjwa wa presha.
Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu.
Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa Chungwa moja lina kiasi cha asilimia 10 ya ‘folic acid’ inayohitajika mwilini kila siku. Madini haya ni muhimu kwa afya ya ngozi na ukuaji wa ubongo kwa ajili ya kuimarisha kumbukumbu na uwezo wa mtu wa kufikiri
Vitamin C iliyomo kwenye chungwa huimarisha uzalishaji wa seli nyeupe ambazo ni muhimu kwa uimarishaji wa kinga ya mwili. Unapokuwa na kinga imara, huwezi kusumbuliwa na magonjwa mara kwa mara, yakiwemo malaria.
Mbali na magonjwa hayo, pia husaidia matatizo ya kizazi,mishipa ya damu, magonjwa ya ngozi, matatizo ya mirija ya uzazi husaidia usagaji wa chakula mwilini pamoja na kutuliza kichefuchefu kwa wajawazito
Ifahamike Chungwa, siyo tu linatoa kinga kwa magonjwa yaliyoainishwa hapo juu, bali pia hutoa kinga hata kwa magonjwa mengine kama vile baridi yabisi (arthritis, rheumatism), pumu, kikohozi, kifua kikuu, nimonia na kisukari. Nakushauri kula machungwa au juisi yake halisi kuanzia leo ili kupata faida hizo.

Hizo ndizo baadhi ya dondoo muhumu za faida za machungwa kwa afya ya mwili wako. 

Usikose kuungana nami katika mfululizo wa makala ya AFYA YA JAMII ili kufahamu mambo mbalimbali kuhusu matunda

Post a Comment

 
Top