0
Chuo Kikuu cha Nairobi kimewafukuza wanafunzi 139 zaidi kwa kushiriki mgomo uliosababisha uharibifu mkubwa wa mali. Wanafunzi hao walitakiwa kuchukua barua za kufukuzwa kutoka kwa msajili wa wanafunzi ifikapo Ijumaa ya wiki hii.
Naibu Chansela wa Chuo hicho Profesa Peter Mbithi amesema hii ni moja wapo ya hatua za kinidhamu dhidi ya wanafunzi walioongoza mgomo huo.
 Kwa sasa Chuo hicho kimefungwa. Jumanne wiki hii wanafunzi 62 walifukuzwa akiwemo Mike Jacobs mgombea wa wadhifa wa Mwenyekiti wa chama cha wanafunzi{SONU} 
.Jacobs alikua mpinzani wa mwenyekiti wa sasa Babu Owino. Polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi baada ya kupata silaha ikiwemo visu vilivyokua na damu hali inayozua hofu ya kuwepo magenge ya uhalifu ndani ya Chuo hicho.

Post a Comment

 
Top