0
Saudi Arabia imejibu tangazo la Iran kwamba raia wake hawataruhusiwa kwenda kuhiji Makka mwaka huu,kwa madai ya kwamba mamlaka ya Saudia imetengeneza vikwazo kwa mahujaji wa Iran kushiriki Hijja hiyo.
Hata hivyo Waziri wa Mambo ya nje wa Saudia Adel al-Jubeir amesema kuwa waumini hao wa Kiislam kutoka nchini Iran,wanahitaji kupewa idhini pia ya kufanya maandamano wakiwa nchiniSaudia jambo ambalo halikubaliki.
Iran inalaumu maafisa wa Saudia kwa vifo vya mamia ya mahujaji wake vilivyotokea mwakajana walipokwenda kuhiji.
Professor Mohammad Marandi kutoka chuo kikuu cha Tehran,anasema wa hoja ya Iran, ni kutaka kujiridhisha kama Mahujaji wake watakuwa salama katika Hijja ya mwaka huu
"Raia wa Iran hawana namna. Maoni ya Wairan ni ya hasira na jazba dhidi ya familia ya Kisaudia. Saudia imewakatalia Wairan matumizi ya Kamera,ambazo ndizo zilizotumika kuonyesha picha za maelfu ya watu waliokufa katika Hijja ya mwaka jana wakiwemo raia wa Iran. Na kwa kuwa Saudia haikulezea mazingira halisi ya vifo hivyo na baadaye ikaomba msamaha,Wairan wanaona bado mazingira hayajawa salama kwao kwa ajili ya Hijja ya mwaka''.
Professor Marandi amesema vurugu zilizosababisha vifo katika Hijja mwaka jana hazikudhibitiwa vyema na serikali ya Saudia
"Saudia ilionyesha bayana kutoheshimu mahujaji,familia zao na kwa miili ya waliokufa, jambo ambalo kwa Wairan halikubaliki. Hivyo Wairan wanataka kujua ni maboresho gani yatafanyika mwaka huu ili waweze kuwa salama zaidi,lakini Saudia hawataki kuweka wazi kwamba ni mabadiliko gani yaliyofanyika,na wakati huo huo viongozi wa dini nchini Saudia wanaamini kuwa Wairan si waumini kamili wa dini ya kiislamu''.

Post a Comment

 
Top