0
Gareth Southgate amechaguliwa rasmi kuwa kocha wa England katika mkataba wa kudumu.
Southgate mwenye umri wa miaka 46 aliwacha wadhfa wake kama mkufunzi wa timu ya England ya vijana wasiozidi miaka 21 mnamo mwezi Septemba baada ya aliyekuwa meneja wa Uingereza Sam Allardyce kujiuzulu baada ya kuhudumu kwa siku 67 pekee.

Aliisaidia Uingereza kushinda mara mbili pamoja na sare mbili kama kaimu mkufunzi na sasa ametia saini kandarasi ya miaka minne yenye thamani ya pauni milioni 2 kwa mwaka.

''Nimefurahia sana kushirikiana na wachezaji katika mechi nne na ndhani kuna vipaji vingi'',alisema.

Post a Comment

 
Top