0
Kiungo wa kati Paul Pogba na Marouane Fellaini watakosa mechi ya kulipiza kisasi ya robo fainali dhidi ya West Ham baada ya kuhudumia marufuku.

Wote wawili walipewa kadi za njano kwa mara ya tano msimu huu wakati timu yao ilipopata sare ya 1-1 siku ya Jumapili.

Mshambuliaji wa West Ham Diafra Sakho ,ambaye alifunga bao katika uwanja wa Old Trafford wikendi iliopita anauguza jeraha la kifundo cha mguu.

Anday Caroll yuko karibu kurudi katika kikosi cha kwanza baada ya kuuguza jeraha la goti huku beki Winston Reid akirudi baada ya kuhudumia marufuku.

Kiungo wa kati wa Manchester United Ander Herrera amesema kuwa itakuwa mechi ya ''kulipiza kisasi'' baada ya timu yake kufeli kuishinda West Ham wikendi iliopita.
Katika mechi nyengine Arsenal itaikaribisha West Ham katika uga wa Emirates

Post a Comment

 
Top