0
Vyombo vya habari nchini Syria vinasema kuwa ndege za jeshi la Israeli, zimerusha makombora mawili kutoka anga ya Lebanon ambayo yalianguka nje ya mji wa Damascus.

Taarifa za kijeshi ziliambia shirika la habari la Sana kuw makombora hayo yalianguka mji wa Sabboura lakini hayakusababiosha maaafa.

Taarifa hizo hazikusema ikiwa chochote kiliharibiwa lakini barabara kuu kutoka Lebanon kwenda Damascus hupitia mji huo.
Jeshi la Israeli halijazungumza lolote.

Ndege hizo zinaamaniwa kushambulia silaha zilizokuwa zinanuiwa kusafirishwa kwenda kwa kundi la Hezbollah nchini Lebanon.

Hezbollah ambayo ilipigana vita vilivyodumu mwezi mmoja na Israeli mwaka 2006, imetuma maelfu ya wapiganaji kumuunga mkono Rais Bashar la-Assad kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.

Mtandao wa habari wenye makao yake mjini London wa Rai al-Youm, ulinukuu taarifa zilizosema kuwa lengo la kwanza lilikuwa ghala la silaha la jeshi la Syria.

Lengo la pili ulikuwa ni msafara wa malori yaliyoaminiwa kusafirisha silaha za kundi la Hezbollah.

Post a Comment

 
Top