0
Kiongozi wa kundi la wapiganaji la Taliban amezungumza kwa mara ya kwanza tangu kuchaguliwa kwake mwezi mei, ambapo ameitaka Marekani kuondoka Afghanistan.
Maulawi Haibatullah Akhundzada amesema uwepo wa Marekani na washirika wake nchini Afghanistan hautaathiri juhudi za makundi ya kijihadi.
Image captionWapiganaji wa Taliban
Amesema kuwa Taliban haitaki kuwa na ukiritimba wa mamlaka, japo akasisitiza kwamba ni Lazima serikali ya Afghanistan ikatize uhusiano wake na Marekani, kama hatua ya kwanza ya mchakato wa amani katika misingi ya sheria za kiislamu.

Post a Comment

 
Top