0
Serikali ya Iraq imesonga mbele katika harakati zake za kutaka kuvikomboa vijiji vinavyoshikiliwa na wapiganaji wa kundi la IS magharibi mwa mji wa Mosul
Vikosi vya wanajeshi wa wakiwa na silaha na helikopita kwa kusaidiana na vikosi vya nga wanaendesha operesheni hiyo ya kukomboa vijiji hivyo.
Mwandioshi wa A BBC aliyeambatana na vikosi vya serikali ameshuhudia silaha na mabomu vikiwa vimetekelezwa na wapiganaji hao,pamoja na magari yenye mabomu na vilipuzi vimefichwa na wapiganaji hao ndani ya majengo.
Eneo la kwanza lililolengwa na vikosi vya serikali katika kukabiliana na IS ni uwanja wa ndege wa Mosul,hata hivyo IS wameendelea kujibu mashambulizi ya mabomu na mabomu yanayodondoshwa na ndege zisizo na marubani drone.
Majeshi ya serikali mwezi uliopita yalifanikiwa kukomboa eneo la mashariki la mji wa Mosul kutoka mikononi mwa wapiganaji wa IS.

Post a Comment

 
Top