0
Waziri mkuu mstaafu wa Ufaransa Manuel Valls amekashifiwa alipokuwa akihamasisha katika kampeni za chama cha kisoshalisti katika uchaguzi mkuu wa kiti cha Urais nchini Ufaransa.
Alipokuwa akihutubia katika ukanda wa Magharibi mwa mji wa Brittany alipigwa kofi na kijana mdogo alipokuwa akisalimia kwa kushikana mikono.
Mlinzi binafsi wa Bwana Valls alimkamata kijana huyo kooni kisha akamtupa chini.
Manuel Valls hajajeruhiwa katika tukio hili.

Post a Comment

 
Top