0
Zaidi ya wafilipino 1000 wameandamana mjini Manila dhidi ya mpango wa kuuzika mwili wa Rais wa zamani aliyefedheheshwa , Ferdinand Marcos, kwenye eneo la mashujaa wa taifa hilo.
Waandamanaji hao walihimili mvua kubwa iliokuwa ikinyesha, na kumuomba rais wa sasa , Rodrigo Duterte, kufuta mpango huo.
Mwaandamanaji mmoja, seneta Risa Hontiveros, amemtaja rais Duterte kuwa adui wa mashujaa wa Ufilipino.
Rais huyo wa awali anatuhumiwa kuhusika katika ufisadi , na ukiukaji wa haki za binaadamu.
Serikali yake ilipinduliwa mwaka wa 1986, na aliaga dunia akiwa uhamishoni miaka mitatu baadaye.

Post a Comment

 
Top