0
Tanzania imeendelea kuwa na neema ya kutembelewa na viongozi wa mataifa mengine baada ya usiku wa kuamkia leo Jumapili kuwasili nchini Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi ambaye alipokelewa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa na viongozi wengine wa kitaifa na kimkoa wa Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi akipunga mkono  kusalimia wananchi waliojitokeza kumlaki mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Mhe. Modi atakuwa nchini kwa ziara ya siku mbili kuanzia tarehe 09-10 Julai, 2016
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akisalimiana na Mhe. Modi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Mhe. Modi mara baada ya kuwasili nchini. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda akisalimiana na Mhe. Modi mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki akisalimiana na Mhe. Modi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege.
Kaimu Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. James Bwana (wa kwanza kulia) akiwaongoza Waheshimiwa Mawaziri Wakuu wakati wa mapokezi.
Kaimu Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. James Bwana (wa kwanza kulia) akiwaongoza Waheshimiwa Mawaziri Wakuu wakati wa mapokezi.

Post a Comment

 
Top