Wafuasi wa Katumbi waliingia mahakamani kwa lazima mjini Lubumbashi anakotarajiwa kufika kusikizwa kwa mara ya pili kesi dhii yake.
Wafuasi wake wanasema tuhuma hizo zimenuiliwa kutatiza kampeni yake ya kisiasa kumrithi rais Joseph Kabila.
Moise Katumbi amethibitisha rasmi siku chache zilizopita kwamba atogemba urais wa nchi hiyo katika uchaguzi utakao fanyika Novemba mwaka huu.
Nyumba yake ilisakwa na walinzi wa serikali siku ya Jumamosi.
Katumbi amekana mashtaka na ameishutumu serikali kwa kutumia njia za kumchafulia jina.
Ubalozi wa Marekani mjini Kinshasa pia umetilia shaka tuhuma hizo.
Rais Joseph Kabila ambaye yupo madarakani tangu mwaka 2001 bado hajabainisha iwapo atajiuzulu mwaka huu kama inavyo takiwa kwenye katiba ya nchi.
Post a Comment