0
Jeshi la Iraq linasema kuwa liko kwenye mapigano makali na wanamgambo wa Islamic State katika eneo la kaskazini mwa mji wa Fallujah.
Wapiganaji wa Islamic State waliojihami kwa makombora wanapigana kutoka kwa makazi na majengo mengine.
Kamanda wa kijeshi alisema kuwa wengi wa wapinaji hao ni raia wa kigeni, ambao hawawezi kukimbia na kujificha miongoni mwa watu na kisha kutoweka,
Mapigano hayo yanaendelea licha ya serikali kutangaza kuwa imeuteka mji wa Fallujah.

Post a Comment

 
Top