Taa hizo zilizo nyekundu kama ilivyo kawaida ya taa za barabarani zinapoashiria mtu au magari kusimama, zinaamanisha kwamba watu zaidi watatembea wakiwa nyuso zao zinaangalia chini, lakini bado wataweza kuona wakati sio salama kutembea.
Kifo cha mtoo mwenye umri wa miaka 15 kililazimisha kuwekwa taa hizo, vyombo vya habari vinaarifu.
Aligongwa kwa treni alipokuwa amezubaa na simu wakati akivuka, polisi inasema.
Wachora ramani wa mji walizingatia sehemu wanapotembea watu wanaotumia simu zao zaidi kama vile vijana na wasafiri, amesema msemaji wa mji Stephanie Lerman.
Watu wanaotembea huku wakizubaa na simu zao wamepewa jina smombies - jina linalotokana na maneno smartphone na zombie.
Jina hilo ni maarufu sana Ujerumani ambako limetajwa kuwa neno la vijana lililotumika zaidi 2015.
Post a Comment