0
VINARA wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Simba SC wanashuka Uwanja wa Kambarage, Shinyanga leo kumenyana na wenyeji, Mwadui FC.
Kwa ujumla Ligi Kuu inaendelea tena leo na mbali na Mwadui na Simba, Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza Toto Africans wataikaribisha Mtibwa Sugar ya Morogoro, Mbeya City watakuwa wenyeji wa Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, African Lyon watakuwa wenyeji wa Tanzania Prisons ya Mbeya Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na JKT Ruvu wataikaribisha Ndanda FC Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.

Post a Comment

 
Top