0
Mahakama moja nchini Afrika Kusini imemhukumu mwanamke mmoja kifungo cha miaka kumi jela kwa kosa la kumteka nyara mtoto mchanga yapata miaka ishirini iliyopita na kumkuza huku akimuamisha kuwa yeye ndiye mama yake mzazi.
Mwanamke huyo sasa ana umri wa miaka hamsini amekana madai ya yanayomkabili ya udanganyifu na utekaji nyara.Muuguzi Zephany anasema mtoto huyo mchanga alinyakuliwa alipokuwa amelala kwenye kitanda kando y mama yake katika hospitali iliyoko mjini Cape Town.
Tuhuma dhidi ya mwanamke huyo zilianza tangu mnamo mwaka jana mara baada ya binti aliye mwiba kuanzisha urafiki baina yake na msichana mdogo aliyekuwa anasoma naye kufanana mpaka kutia fora.Uchunguzi wa vinasaba ulipofanywa, watoto hao waligundulika kuwa ni ndugu.
Hakimu Hlope alimwambia mshtakiwa kwamba ameidanganya mahakama yake na haonekani kujutia kosa lake.

Post a Comment

 
Top