0


Mahakama moja nchini Kenya imetoa uamuzi kwamba polisi wa utawala waliteka nyara wakili Willie Kimani, mteja wake na dereva wa teksi.
Wote watatu waliteswa na kuuawa, tukio ambalo lilisababisha maandamano nchini Kenya dhidi ya mauaji yanayotekelezwa na polisi.
Mahakama ya juu nchini kenya imegundua kwamba wakili Willie Kimani, mteja wake Josphat Mwenda and dereva wa teksi Joseph Muiruri walitekwa nyara mwezi Juni tarehe 23, wakazuiliwa katika kituo cha polisi ambacho hakijachapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali na ambacho kilitumika kuwatesa na kuuawa kikatili.
Mahakama hiyo pia imeamuru kwamba wakili Willie Kimani, hasa kwa sababu za vile aliuawa na mwili wake kutupwa mtoni, atambuliwe kama mtetezi wa sheria kama njia mwafaka ya kumkumbuka.
Jaji pia alifahamu kwamba uchunguzi wa mauaji haya uliingiliwa kati na washukiwa ambao walikuwa wamejitolea kusambaratisha haki kutendeka.
Chama cha wanasheria nchini Kenya kilikuwa kimewasilisha malalamiko mahakamani kikitaka polisi waseme kule wakili, mteja wake na dereva wa teksi waliko wakati walipopotea.
Maafisa wanne wa polisi wa utawala tayari wameshtakiwa juu ya mauji haya.

Post a Comment

 
Top