0
Kiongozi mwanamapinduzi wa Cuba Fidel Castro anasherehekea kutimiza miaka 90 tangu kuzaliwa kwake.
Mzee huyo, aliyetawala kisiwa hicho kwa zaidi ya miaka 50, hajaonekana hadharani kwa miezi mingi na bado haijabainika iwapo atajitokeza leo.
Ingawa Cuba imebadilika sana tangu kakake Raul achukue hatamu miaka minane iliyopita, na ushawishi wa Fidel umeshuka, bado anaenziwa sana na raia wengi wa Cuba.
Hakuna hafla yoyote rasmi iliyopangiwa kufanywa, lakini Rais wa Venezuela Nicolas Maduro, taifa mshirika wa karibu wa Cuba, amewasili Havana kushiriki katika sherehe hizo.
Fidel Castro mwaka 2010Image copyrightGETTY IMAGES
Image captionFidel Castro amekuwa akirejea chuo alichosomea na kutoa mihadhara
Mtengenezaji sigara maarufu raia wa Cuba ametayarisha msokoto mrefu zaidi wa sigara duniani kwa heshima ya Castro.
Msokoto huo una urefu wa mita 90.

Post a Comment

 
Top