0
China inafanya mazoezi ya kijeshi kusini mwa bahari ya China siku chache kabla ya uamuzi muhimu wa mahakama kuhusu mzozo ulio eneo hilo la bahari.
Mazoezi hayo yanafanyika karibu na visiwa vinavyozozaniwa vya Paracel.
Mahakama ya haki mjini Hague inatarajiwa kutoa uamuzi wake wiki ijayo katika kesi iliyowasilishwa na Ufilipino.
Image copyrightREUTERS
China tayari imesema kuwa haitakubali uamuzi huo.
Gazeti moja la serikali The Global Times linasema kuwa China inastahili kujiandaa kukabiliana na Marekani.

Post a Comment

 
Top