0
Virusi vya ugonjwa wa zika vinaweza kusambaa na kuingia Ulaya wakati wa majira ya kiangazi ,ijapokuwa uwezekano wa mlipuko wake uko chini kwa wastani, kulingana na shirika la afya duniani.
Maeneo ambayo yamo hatarini ni yale ambayo mbu aina ya Aedes huenda wakasambaza virusi hivyo ,kama vile pwani ya bahari nyeusi huko Urusi,Georgia na kisiwa cha Madeira.
WHO linayataka mataifa kuyaondoa maeneo yanayozalisha mbu na maeneo yake na kuhakikisha kuwa watu hususan waja wazito wana habari kuhusu athari za ugonjwa huo.
Image copyrightAP
Image captionMaafisa wa afya wakikabiliana na virusi vya Zika
Shirika hilo linasema kuwa mataifa mengi ambayo huenda yakaathiriwa yamejiandaa kukabiliana na visa vipya na kukabiliana navyo kwa haraka,lakini mataifa mengine yatalazimika kukabiliana na ugonjwa huo.

Post a Comment

 
Top