0
Chama kikuu cha upinzani nchini Zambia kimepeleka kesi mahakamani kupinga ushindi wa Rais Edgar Lungu uliofanyika mapema mwezi huu.
Mgombea wake wa urais Hakainde Hichelema, aliiambia BBC kuwa uchaguzi huo uliibwa kutoka kwake na haukuonyesha matakwa ya watu wa nchi humo.
Chama chake cha National Development (UNDP) kimemuandikia spika wa bunge, kikimtaka achukue wadhifa wa urais hadi uamuzi wa mahakama utolewe.
Tume ya uchaguzi nchini Zambia ilikuwa imemtangaza Lungu kuwa mshindi kwa asilimia 50.35 huku Hichilema akipata asilimia 47.67 na kusisitiza kuwa uchaguzi ulikuwa wa haki.
Bwana Lungu alimshinda Hichilema uchaguzi uliotangulia mwaka uliopita kwa chini ya kura 28,000.

Post a Comment

 
Top