0
Watu nchini Peru wanapiga kura katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais.
Kura za maoni zinaonyesha kuwa wagombea wote wawili, Keiko Fujimori na Pedro Pablo Kuczynski, karibu wako sare katika uchaguzi wa leo.
Image copyrightAP
Image captionKeiko Fujimori
Bibi Fujimori, wa mrengo wa kulia, aliongoza katika duru ya kwanza mwezi Aprili.
Lakini Bwana Kuczynski, aliyewahi kufanya kazi katika Benki ya Dunia, naye amesonga mbele.
Image copyrightAFP
Image captionPedro Pablo Kuczynski
Bibi Fujimori ni mtoto wa rais wa zamani, Alberto Fujimori, ambaye amefungwa kwa kutenda uhalifu dhidi ya binaadamu.
Amesema swala muhimu ni kupambana na uhalifu.
Bwana Kuczynski anasema, atatumia uzoefu wake katika uchumi wa kimataifa, kuchangamsha uchumi wa Peru uliozorota.

Post a Comment

 
Top